NI KATIKA SEMINA YA MAAFISA WA VIKOBA PAMOJA NA WANA KIKUNDI MKOANI RUKWA - MAISHA ONLINE BLOG

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, June 6, 2015

NI KATIKA SEMINA YA MAAFISA WA VIKOBA PAMOJA NA WANA KIKUNDI MKOANI RUKWA



Mkuu wa wilaya ya nkasi mh. Iddi kimanta  Amewataka  wanachama wa VICOBA (village community bank)  kuzidi kujiimarisha katika vikundi vyao  ili kufukia malengo kusudiwa
Akizungumza kwaniba ya mkuu wa mkoa kwenye  semina ya mpango wa vicoba kwa maafisa wa mkoa wa rukwa ulio jumuisha maafisa wa halmashauri zote za sumbawanga mh kimanta amesema  vikundi hivi vinaumuhimu mkubwa katika jamii kwani lengo kubwa la kuanzishwa kwake ni kusaidia wanajamii kiuchumi na katika shughuli mbalimbali za jamii
Kimanta ameviasa vikundi hivi kutotoafulsa kwa wanasiasa  kuvitumia kama jukwaa la kunadi sera zao hasa katika kipindi hiki cha kampain tunapoelekea uchaguzi mkuu
Aidha kwa upande wake bw. aldo mfinde ambaye ni mratibumtendaji  wa asasi ya UYACODE – Taifa  amezifafanua  faida za kujiunga na vikoba  kuwa ni pamoja na kujiwekea akiba kubwa itakayo wawezesha kupata mikopo mikubwa,
Faida nyingine ni mwana kikundi kujijengea tabia ya kuweka akiba kila wiki  ambayo itampa tija kubwa kwa maendeleo yake na jamii
Banki hii ya kijamii vijijini ni mpango unaotumia mfumo wa MMD (MATA MASU DUBALA)  ulioanzishwa na shirika la Care internetiona  nchini niger 1991  unatoa fulsa ya mwanajamii kumiliki mtaji na riba tofauti na mifumo mingine ya ukopeshaji fedha ambapo umiliki ni wa mkopeshaji na mkopaji anakuwa kama chombo cha  kumzalishia faida mkopeshaji
 TAZAMA PICHA ZA WAHIRIKI HAPA CHINI



















No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot