VIONGOZI WA AFRIKA KUZINDUA KANDA MPYA YA SOKO LA PAMOJA - MAISHA ONLINE BLOG

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, June 10, 2015

VIONGOZI WA AFRIKA KUZINDUA KANDA MPYA YA SOKO LA PAMOJA

Viongozi mataifa 26 ya Kiafrika wamekutana Misri  Jumatano hii (10.06.2015) kusaini makubaliano ya kuanzisha soko la pamoja litakalojumuisha nusu ya bara la Afrika na kuwahudumia watu milioni 625. African Union Development Planning in Abidjan
Kusainiwa makubaliano hayo ya biashara huru kati ya jumuiya tatu TFTA, kunahitimisha majadiliano yaliyodumu miaka mitano yenye lengo la kuunda mfumo wa ushuru wa upendeleo ambao utarahisisha usafirishaji wa bidhaa kutoka mataifa wanachama.

Makubaliano hayo yanajumlisha maslahi ya jumuia ya Afrika Mashariki EAC, jumuiya ya maendeleo ya mataifa ya kusini mwa Afrika SADC, na jumuiya ya soko la pamoja la mataifa ya mashariki na kusini mwa Afrika COMESA, ambazo mataifa yake yana pato la jumla la ndani la dola trilioni moja.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot