Kusainiwa makubaliano hayo ya biashara huru kati ya jumuiya tatu TFTA, kunahitimisha majadiliano yaliyodumu miaka mitano yenye lengo la kuunda mfumo wa ushuru wa upendeleo ambao utarahisisha usafirishaji wa bidhaa kutoka mataifa wanachama.
Makubaliano hayo yanajumlisha maslahi ya jumuia ya Afrika Mashariki EAC, jumuiya ya maendeleo ya mataifa ya kusini mwa Afrika SADC, na jumuiya ya soko la pamoja la mataifa ya mashariki na kusini mwa Afrika COMESA, ambazo mataifa yake yana pato la jumla la ndani la dola trilioni moja.
No comments:
Post a Comment