
Zaidi ya nyumba 200 zimezingirwa na maji
katika Manispaa ya Mtwara Mikindani kufuatia mvua zinazoendelea
kunyesha na kusababisha hasara kubwa ambayo thamani yake bado
haijajulikana.
Kufuatia hali hiyo Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima
Dendegu ametoa saa 24 kwa wataalam kuhakikisha wanayaondoa maji ndani
ya makazi ya watu.
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Wilaman Ndile amemwambia
mkuu huyo wa mkoa alipotembelea maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko hayo
kuwa zaidi ya nyumba 200 zimezingirwa na maji katika mitaa mbalimbali ya
manispaa hiyo.
No comments:
Post a Comment